< Katwa Nono Katwa 2 >

1 Nanaya wui une a Yahudawa wadin ubuki kusana (Upentakos) mine, anan yinu sauyenu wadi kitikirum nanya Urshalima.
Siku ya Pentekoste ilipofika, waumini wote walikuwa wamekusanyika pamoja.
2 Nin kubi kwak ilanza ufunu likara inin lanza liwui unuzu kitene kana. Anit vat kikane na iwa sosin ku ilenza ukara liwuiye.
Ghafla, sauti ikasikika kutoka angani; sauti iliyokuwa kama ya upepo mkali, ikajaza ile nyumba yote walimokuwa wamekaa.
3 Kikanere ntutun inin yene Ufunu Ulau kitene aniti mine nafo ula. Tilem ule so kitenen kogye, umon nanya mine nuzu ada kitenen litin nanan yinnu sanu.
Kisha, vikatokea vitu vilivyoonekana kama ndimi za moto, vikagawanyika na kutua juu ya kila mmoja wao.
4 Vat mine kulo nin Funu Ulau, inin tinna bellu tipipin bgarden, nafo na Ufunu Ulau wa dursuzo nanin.
Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema lugha mbalimbali kadiri Roho alivyowawezesha.
5 Kubi kone, among Ayahudawa wa sosin nanya Urshalima iniydge wadi anan fiwu Kutelleri na iwa dak nitiniti gbardan.
Na huko Yerusalemu walikuwako Wayahudi, watu wamchao Mungu, waliotoka katika kila nchi duniani.
6 Dana ilanza liwui umosin ufun, anite tinna ipitiruno kidowo kiti kirum kikana anan yinnu sauyenu wadiku. lipitirin nanite wa su umamak bara kogha nanya na nananyinu sauyenu wadin belu tipipin mine.
Waliposikia sauti hiyo, kundi kubwa la watu lilikusanyika. Wote walishtuka sana kwani kila mmoja wao aliwasikia hao waumini wakisema kwa lugha yake mwenyewe.
7 Ilanza umamaki i woro nin na timine, ''Na vat alele na idin lire ina nuzu kusarin Galiliari iyiziari yinno to ti lembite?
Walistaajabu na kushangaa, wakisema, “Je, hawa wote tunaowasikia wakisema hivi, si wenyeji wa Galilaya?
8 Vat bite tidin lanzu nanin liru nin ti pipinbite na ina maru nari mun,
Imekuwaje, basi, kwamba kila mmoja wetu anawasikia wakisema kwa lugha yake mwenyewe?
9 among bite na nuzu kusarin Patia nin Midia au Elam, among nanya bite nuzukusarin Umesopotamia, Uyahudia, Cappadocia, Pentus nin Uasia.
Baadhi yetu ni Waparthi, Wamedi na Waelami; wengine ni wenyeji wa Mesopotamia, Yudea, Kapadokia, Ponto na Asia,
10 Kikane among anit wa nuzu kusarin Firizia nin Panfilia, Umasar nin kusarin kagbirin libia idadas nin kagbirin Cirian. Kikane among bite amara Urshalima unuzun Roma.
Frugia na Pamfulia, Misri na sehemu za Libya karibu na Kurene; wengine wetu ni wageni kutoka Roma,
11 Umunu nin na Yahudawe, au a Yahudawa na ina yinin nin nilemong na arik a Yahudawe yinamung. Among bite nuzu kusarin Island na Krete nin kusarin ka gbirin Arabia. Bari yan-aarin ta ale anite din belu tipipin bite kitene nilemong na Kutelle nasua?
Wayahudi na watu walioongokea dini ya Kiyahudi; wengine wametoka Krete na Arabia. Sisi sote tunasikia wakisema kwa lugha zetu wenyewe mambo makuu ya Mungu.”
12 Anite wa lanza umamaki na iwa yininin yari neba itin na tiru natimine “Ile imone yaria?”
Wote walishangaa na kufadhaika huku wakiulizana, “Hii ina maana gani?”
13 Among many mine imagining wish nanin lninworo, “Ale white din lirunafo isono intoro moninmolo naninkan!”
Lakini wengine wakawadhihaki wakisema, “Watu hawa wamelewa divai mpya!”
14 Bitrus fita alirina kan aworo anan lipitin; nanite, “Anin anan Yahudia nin nalenaisosin in Urshalima, ma Latiszannin vat mine, ima benlinminu ilemong idin yenju.
Lakini Petro alisimama pamoja na wale kumi na mmoja akaanza kuwahutubia watu kwa sauti kubwa: “Ndugu Wayahudi nanyi nyote mnaokaa hapa Yerusalemu, sikilizeni kwa makini maneno yangu.
15 Among nanya mine din du untoro molo nari nanere ba ai nene kubi karfe tarari nin kudin, anit alele sonon utoro nin kokubi nin lolire ba!
Watu hawa hawakulewa kama mnavyodhani; mbona ni saa tatu tu asubuhi?
16 Bara nanin elemon na iyene kiti bite ina malin yertinu ku annabi Joel na belin uworu.
Ukweli ni kwamba jambo hili ni lile alilosema nabii Yoeli:
17 Kubi nayiru nimalin gye, Ima niUfunu Ulau kiti nanite vat, ason nin na shono mine ma belu anite kadura ningye, Inani anyana mine uyejun, akune inma ninanin amoron yenju kiti.
Katika siku zile za mwisho, asema Bwana, nitawamiminia binadamu wote Roho wangu. Watoto wenu, wanaume kwa wanawake, watautangaza ujumbe wangu; vijana wenu wataona maono, na wazee wenu wataota ndoto.
18 Kubi nayira ne ima ni Ufunu Ulau kiti nono nin, inan bele anit tipipin nin.
Naam, hata watumishi wangu, wanaume kwa wanawake, nitawamiminia Roho wangu, siku zile, nao watautangaza ujumbe wangu.
19 Imati imong idiya ti kitene kani, nin kutin idurso minu imong icine naimase. Kikane kutin, mmi nin ula nin cin vat niti.
Nitatenda miujiza juu angani, na ishara chini duniani; kutakuwa na damu, moto na moshi mzito;
20 Kite kane ma ti uwui uti bibit kiti na nit nin pui uti ushine nafo kiti mine. Umong ine mati ma innin dak ida, Men Kutelle manin dak ida su mawusuwusu. kitin konyge.
jua litatiwa giza, na mwezi utakuwa mwekundu kama damu, kabla ya kutokea ile siku kuu na tukufu ya Bwana.
21 Iminin ma tucu anit alena idin yici in bin nanin.'”
Hapo, yeyote atakayeomba kwa jina la Bwana, ataokolewa.
22 Bitrus tin alau ubin in lire,”Nuana nin a Iraila latizani! Kubi kona Yesu nazaret wa di nan yginu Kutelle na dura minu amere na tuu gye a su matiza ma zikiki mane maana maanaduro amere KutelleAnin natimene yiru nin limo umongye kidene.
“Wananchi wa Israeli, sikilizeni maneno haya! Yesu wa Nazareti alikuwa mtu ambaye mamlaka yake ya kimungu yalithibitishwa kwenu kwa miujiza, maajabu na ishara Mungu alizofanya kati yenu kwa njia yake, kama mnavyojua.
23 Nin nanin iyiru, anin gyere na nakwa Yesu ku kiti nanan ni vira me. Nin nanin Kutelle na malin yinu mu, amini yiru nin nimone. Inin taa anit alena iyiru nin udoka Kutelle ba anan molo Yesu ku. Inani wa kotin gye akusa kite kuca.
Kufuatana na mpango wake mwenyewe Mungu alikwisha amua kwamba Yesu angetiwa mikononi mwenu; nanyi mkamuua kwa kuwaachia watu wabaya wamsulubishe.
24 Amini na kuu, Kutelle na feagye tutun, bara nanin ukul wagya kifo gye kutinba. Kutelle nati Yesu afita tutun.
Lakini Mungu alimfufua kutoka wafu akamwokoa katika maumivu ya kifo kwa maana haingewezekana kabisa kifo kimfunge.
25 Tuntuni ugo Dauda na yertin kitenen Missiah aworo,”In yiru fewe ku Kutelle, uma lanzi kokome kubi, idi kusa nin mina ima lanzu infiu na le na iin su ivira nin mi ba.
Maana Daudi alisema juu yake hivi: Nilimwona Bwana mbele yangu daima; yuko nami upande wangu wa kulia, na hivyo sitatikisika.
26 Bara nanin kibinai nin ma ti pau, konin kul nin, inyiru uma buni.
Kwa hiyo, moyo wangu ulifurahi; tena nilipiga vigelegele vya furaha. Mwili wangu utakaa katika tumaini;
27 Uma cini kikana anan kule diku ba. Na uma kuru cin kidawo nin bijuba, bara idi ni fi nin dortu fi nin su ubiyanya' (Hadēs g86)
kwa kuwa hutaiacha roho yangu katika kuzimu, wala kumruhusu mtakatifu wako aoze. (Hadēs g86)
28 Una malin benle tibou tona ima dfunu ina taa ulai tutun. Umati kibinai nin ti paubara udi nin me sa ligan.
Umenionyesha njia za kuufikia uzima, kuwako kwako kwanijaza furaha!
29 Nuana, nwasa nlira nanghinu sa fiu kitenen kaa bite Dauda: awa ku ikuru ikasaghe, kissek me di nanghirik udak kitimone.
“Ndugu zangu, napenda kuwaambieni waziwazi juu ya mambo yaliyompata Daudi, babu yetu. Yeye alikufa, akazikwa, tena kaburi lake liko papa hapa petu mpaka leo.
30 Bara nani, awadi gono katwa Kutelleri ayiro nwo Kutelle wasughe issilin, nworu ama ceo umong nanya fisudu me kitenen kutet tigo.
Lakini kwa vile Daudi alikuwa nabii, alijua kuwa Mungu alimwapia kiapo kwamba atamtawaza mmoja wa uzawa wake kuwa mfalme mahali pake.
31 Awa yene ile imone, alira nbellen fitun Kristi nanya nkul, 'Na iwa shawa ninghe nanya kisseke ba, ana na kidowo me wa yene ubiju ba.' (Hadēs g86)
Daudi aliona kabla mambo yatakayofanywa na Mungu na hivyo akasema juu ya ufufuo wa Kristo wakati aliposema: Hakuachwa kuzimu, mwili wake haukuoza. (Hadēs g86)
32 Nin kidun ame Yesu na kuu. Kutelle na fegye tutu. Vat arik anan dortu gyer, tiru mung bara tina yeneyge.
Basi, Mungu alimfufua huyo Yesu na sisi sote ni mashahidi wa tukio hilo.
33 Kutelle na Yesu kutet kudiya amini na ce gye incara ulime me asu ti goo nin Cife. Amini na niri Ufunu Ulau unere taa idin yenju nin lan ze.
Yesu aliinuliwa juu mpaka upande wa kulia wa Mungu, akapokea kutoka kwa Baba ile zawadi aliyoahidi yaani Roho Mtakatifu; na mnachoona sasa na kusikia ni mmiminiko wa huyo Roho.
34 Tiyiru kap Dauda wadin liru litimere b, bara ame Dauda na duo kitene ba nafo Yesu, nin nanin wang. Dauda litime na be3ling uliru kitene Yesu amere Missiah. Cikilari Kutelle na bwabelin Cikilari nin Missia, su tigo in cara ulime nin
Maana Daudi mwenyewe, hakupanda mpaka mbinguni; ila yeye alisema: Bwana alimwambia Bwana wangu: Keti upande wangu wa kulia,
35 Ma inin kata likara nanan ni vira nin.”
hadi nitakapowafanya adui zako kibao cha kukanyagia miguu yako.
36 Bitrus nin mala uliru me aworo,”idinin suo iyini vat a Israila Kutelle nati Yesu ku asuo Cikilari nin Missiah, Yesu unere ulena iwa kotinyge ti kusa kitene kuca inin mologye.
“Watu wote wa Israeli wanapaswa kufahamu kwa hakika kwamba huyo Yesu mliyemsulubisha ninyi, ndiye huyo ambaye Mungu amemfanya kuwa Bwana na Kristo.”
37 Dana anite lanza elemon na Bitruse nin nanan kadura benle, iyino ita kulapi, inin woro nanin iyeri tima ti nene?
Basi, watu waliposikia hayo, walichomwa moyo, wakawauliza Petro na wale mitume wenzake: “Ndugu zetu, tufanye nini?”
38 Bitrus nin kwana nani, vat mine icin kulapi min, Andi iyinna nin yise tima su minu ubaptizma. Kutelle ma ma yashu nin kulapi mine, ani niminu Ufunu Ulau Me.
Petro akajibu, “Tubuni na kila mmoja wenu abatizwe kwa jina la Yesu Kristo ili mpate kuondolewa dhambi zenu na kupokea ile zawadi ya Roho Mtakatifu.
39 Kutelle na malin su likawali amanimunu har nin nono mine nin na nela iyina nin Yesu nin nalena idi pii kusari kikane. Cikilari bite Kutelle mani Ufunu Ulau nin na lena a yicila gye uniti me.
Maana, ahadi ile ilikuwa kwa ajili yenu, kwa ajili ya watoto wenu, kwa ajili ya wote wanaokaa mbali; na kwa ajili ya kila mtu ambaye Bwana Mungu wetu atamwita kwake.”
40 Bitrus wa liru kang kiti mine, Anin woro nanin “Tirinon Kutelle anan shawa [yape]minu bara awan nimunu kikanci nafo ale anite na inanari Yesu ku.
Kwa maneno mengine mengi, Petro alisisitiza na kuwahimiza watu akisema, “Jiokoeni katika kizazi hiki kiovu.”
41 Anite na iwa yinin sa yenu nin liru Bitrus iwa ti ubaptisma. Anan yinu sa uyenu kpina kan har timui ti tat, unwui une.
Wengi waliyakubali maneno yake, wakabatizwa. Watu wapatao elfu tatu wakaongezeka katika kile kikundi siku hiyo.
42 Eliu ubun nanya indurtu nilemon na iwa dueso nani. Iwa din ga uzursuzu kookome kubi inin namong anan yinu sauyenu kikane ici liu emonli ligowe nin nin ti lira ligowe kiti kirem kolome liri.
Hawa wote waliendelea kujifunza kutoka kwa mitume, kuishi pamoja kidugu, kumega mkate na kusali.
43 Vat anite na iwa din nanya Ushalima ifio kifo nanin nin kata ka zikiki na almajaraye wadin sua nin lisa yesu.
Miujiza na maajabu mengi yalifanyika kwa njia ya mitume hata kila mtu akajawa na hofu.
44 Vat na rika na iwa yinin warsu ko nyan ligowe. Inin leu ubun kosusu nin ligawe.
Waumini wote waliendelea kuwa kitu kimoja na mali zao waligawana pamoja.
45 Unuzu kubikubi kogha lese anen me adasamu kiti nanan katawe. Nin nimong ile na kogha nadimun
Walikuwa wakiuza mali na vitu vyao kisha wakagawana fedha kadiri ya mahitaji ya kila mmoja.
46 Ko kishi iwa din zursusu kiti lira kikaneIwa li umonli ligowe ni picu nilari nilari. kubi kona isu nanin ni binai mine taah pau [lanza man ini niza ilemong na kogha diman lgowe.
Waliendelea kukutana pamoja kila siku Hekaluni. Lakini wakati wa kumega mkate, walikutana katika nyumba zao na wakakishiriki chakula hicho kwa furaha na moyo mkunjufu.
47 Dana su nani, ie ubung zazunu Kutell. Nin nanin vat anit Urshalima nananin ubagirma kubikona imong ine wa linbub ghe anan biye kwina kang kolome liri bara use utucu kusari kulapi mine.
Walimtukuza Mungu, wakapendwa na watu wote. Kila siku Bwana aliwaongezea idadi ya watu waliokuwa wakiokolewa.

< Katwa Nono Katwa 2 >