< Katwa Nono Katwa 11 >

1 Nen, niono kadura, nan nuana, alenge na iwa di nanyan Yahudiya lanza alumai tutun nsere uliru Kutelle.
Mitume na ndugu kule Yudea walisikia kwamba watu wa mataifa mengine pia walikuwa wamelipokea neno la Mungu.
2 Kubi na Bitrus ndaa Urushalima, inung alenge na idi anan kallu kucuru sughe kayasu;
Basi, Petro aliporudi Yerusalemu, wale Wayahudi waumini waliopendelea watu wa mataifa mengine watahiriwe, walimlaumu wakisema:
3 Iworo “Fe dinsu ligo nin na nan salin kalizu kucuru, umini din su kileo nanghinu!”
“Wewe umekwenda kukaa na watu wasiotahiriwa na hata umekula pamoja nao!
4 Ame Bitrus cizina ubellu nani nimon inda na idi, a woro.
Hapo Petro akawaeleza kinaganaga juu ya yale yaliyotendeka tangu mwanzo:
5 Meng wadi nlirang nanya kagbiri Njoppa, nta amoro nwui nbellen kukuzun na kuwa tollu, nafo kupee kupash, itoltuna unuzu kitene kani, nin nasari anas, ku da tolo kiti nighe.
“Siku moja nikiwa nasali mjini Yopa, niliona maono; niliona kitu kama shuka kubwa likishushwa chini kutoka mbinguni likiwa limeshikwa pembe zake nne, likawekwa kando yangu.
6 nceo iyizi nighe ku, nkpiliza kitene, nyene inawa nabunu anas kutyin, inawa ididia kusho, in wunnu naburi, nan nanyin kitene kani.
Nilichungulia ndani kwa makini nikaona wanyama wenye miguu minne, wanyama wa mwituni, wanyama watambaao na ndege wa angani.
7 Nnin lanzu liwui li woroiyi “Fita Bitrus, mollo ulii!”
Kisha nikasikia sauti ikiniambia: Petro amka, chinja, ule.
8 Meng woro na nanere ba, Cikilari, bara na imomon nsalin lau sa indinong nsa pira unnu ninghe ba.”
Lakini mimi nikasema: La, Bwana; maana chochote kilicho najisi au kichafu hakijapata kamwe kuingia kinywani mwangu.
9 Ama liwuiye kawa tutun unuzu kitene kane, “Ile imon na Kutelle nbelle idi lau, nafe nwa yiccila inin indinong ba.
Ile sauti ikasikika tena kutoka mbinguni: Usiviite najisi vitu ambavyo Mungu amevitakasa.
10 Ile imone wasu nani udu titat, nin nani vat nimone iwa kpilin mun udu kitene kane tutung.
Jambo hilo lilifanyika mara tatu, na mwishowe vyote vilirudishwa juu mbinguni.
11 Na nin molu kubi ba, kikane among anit natat, wa yisssin nbun kilare na nwa duku, itoo nani unuzun Kaisariya udak kiti ninghe.
Ghafla, watu watatu waliokuwa wametumwa kwangu kutoka Kaisarea waliwasili kwenye nyumba niliyokuwa nakaa.
12 Uruhu tayi nnya nanghinu, na nwa su maferuferu kiti mine ba. Nuana nane kutoci ne nya nanmi, udu nanya kilari nniti une.
Roho aliniambia niende pamoja nao bila kusita. Hawa ndugu sita waliandamana nami pia kwenda Kaisarea na huko tuliingia nyumbani mwa Kornelio.
13 A belle nari yanda na ayene anan kadura Kutelle nanya kilari me, inin woro “Too anit udu Ujoppa idanin Bitrus ulenge na idin yiccughe Simon.
Yeye alitueleza jinsi alivyokuwa amemwona malaika amesimama nyumbani mwake na kumwambia: Mtume mtu Yopa akamwite mtu mmoja aitwaye Simoni, kwa jina lingine Petro.
14 Ame ma liru nanghinu nbellen kadura kanga na ubase utucufe nin vat kilari fe.”
Yeye atakuambia maneno ambayo kwayo wewe na jamaa yako yote mtaokolewa.
15 Na ncizina uliru nanghinu, Uruhu ulau tolo kitene mine nafo na uwa tolu nghireke nin cizinue.
Na nilipoanza tu kuongea, Roho Mtakatifu aliwashukia kama alivyotushukia sisi pale awali.
16 Meng lizuno nin lirun Cikilari, na awa woro, “Yuhana ame wa shintizin anit nin nmyen; ama anung ima shintizunu minu nanya Ruhu ulau.”
Hapo nilikumbuka yale maneno Bwana aliyosema: Yohane alibatiza kwa maji, lakini ninyi mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu.
17 Andi Kutelle wa ni nani ufillu nafo na ana ninari kube nati wa yinnin nin Cikilari Yesu Kristi, menghari wadi nworu in yissin gambalang nin Kutelle?”
Basi, kama Mungu amewapa pia watu wa mataifa mengine zawadi ileile aliyotupa sisi tulipomwamini Bwana Yesu Kristo, je, mimi ni nani hata nijaribu kumpinga Mungu?”
18 Na ilanza ile imone, na itardaghe uliru ba, iwana zazin Kutelleri, iworo, “Kutelle nani Awurmi likara nsunu naliapi wang.”
Waliposikia hayo, waliacha ubishi, wakamtukuza Mungu wakisema, “Mungu amewapa watu wa mataifa mengine nafasi ya kutubu na kuwa na uzima!”
19 Bara nani anan yinnue na iwa sono uniu ulenge na uwa cizin kubin Istifanus wati nani imala kiti vat unuzun Urushalima-alenge na inya ido pit udi duru Ufinikiya. Iwa bellu ubeleng nlirun Yesu kiti na Yahudawari cas, ana umon tutung ba.
Kutokana na mateso yaliyotokea wakati Stefano alipouawa, waumini walitawanyika. Wengine walikwenda mpaka Foinike, Kupro na Antiokia wakihubiri ule ujumbe kwa Wayahudi tu.
20 Ama among anit, unuzun Saipirus nin Serene, wadak Antakiya ida su a Hilinawa nin wazin Ciklari Yesu.
Lakini baadhi ya waumini waliotoka Kupro na Kurene, walikwenda Antiokia wakautangaza huo ujumbe kwa watu wa mataifa mengine wakiwahubiria ile Habari Njema juu ya Bwana Yesu.
21 Tutung ucaran Cikilari wayita ligowe nanghinu; anit gbardang gitirno iyinna idofino Cikilare ku.
Bwana aliwasaidia na idadi kubwa ya watu iliamini na kumgeukia Bwana.
22 Ubelleng mine da duru atuf nanan kilarin lira in Urushalima; inani wa tuu Barnabas ku udu Antakiya.
Habari ya jambo hilo ikasikika kwa lile kanisa la Yerusalemu. Hivyo wakamtuma Barnaba aende Antiokia.
23 Na awa dak ada yene ufillu Kutelle, ayi poaghe; anin na nani likara nibinayi nworu iso ligowe nanyan Cikilare nin nibinayi mine vat.
Alipofika huko na kuona jinsi Mungu alivyowaneemesha wale watu, alifurahi na kuwahimiza wote wadumu katika uaminifu wao kwa Bwana.
24 Bara awadi unit ugegeme nin Ruhu ulau a uyinnu sa uyenu ni Yesu, iwase ukpinu nanit gbardang kitin Cikilare.
Barnaba alikuwa mtu mwema na mwenye kujaa Roho Mtakatifu na imani. Kundi kubwa la watu lilivutwa kwa Bwana.
25 Barnabas tunna anuzu udun Tarsus adi pizuru Shawulu ku.
Kisha, Barnaba alikwenda Tarso kumtafuta Saulo
26 Na awa seghe, amini wa dak ninghe Antakiya. Uni waso nafo nenge, nanya likus iwa sozo ligowe kilari nlira idursuzo anit gbardang. Iwa cizin uyicu nnono kadure anan dortu Kutelle in Antakiyari.
Alipompata, alimleta Antiokia. Nao wote wawili walikaa na lile kanisa kwa mwaka wote mzima wakifundisha kundi kubwa la watu. Huko Antiokia, ndiko, kwa mara ya kwanza, wafuasi waliitwa Wakristo.
27 Nanya nayiri ane among a Anabawa wa dak Antakiya unuzun Urushalima.
Wakati huohuo, manabii kadhaa walikuja Antiokia kutoka Yerusalemu.
28 Umong mine unan lissan Agabus, fita ayissina a durso nnuzun Ruhu a woro kukpong kudya ma malu uyii ulele vat. Ile imone wase nayirin Kiladiyus.
Basi, mmoja wao aitwaye Agabo alisimama, na kwa uwezo wa Roho akabashiri kwamba kutakuwa na njaa kubwa katika nchi yote (Njaa hiyo ilitokea wakati Klaudio alipokuwa akitawala).
29 Bara nani, nono Katwawe tunna iworo ituu nin bunu udu kiti linuana in Yahudiya, nafo na kogha ma yinnu.
Wale wanafunzi waliamua kila mmoja kwa kadiri ya uwezo wake apeleke chochote ili kuwasaidia wale ndugu waliokuwa wanaishi Yudea.
30 Iwa su nani; itoo nin nikurfung kiti na kukune nacaran Barnabas nin Shawulu.
Basi, wakafanya hivyo na kupeleka mchango wao kwa wazee wa kanisa kwa mikono ya Barnaba na Saulo.

< Katwa Nono Katwa 11 >