< Katwa Nono Katwa 10 >

1 Nene umong unit waduku nanya kagbirin Siseriya, nin lissan Konoliyus, kusoja kudyawa ligonzin na Italiya.
Kulikuwa na mtu mmoja huko Kaisarea aitwaye Kornelio, Jemadari wa kikosi kimoja kiitwacho “Kikosi cha Italia.”
2 Awadi unit in biya kang, urika na nawadin dortu Kutelle nin kilari me vat; awa nizu anit na Yahudawa ikubu gbardang anin suzu inlira kiti Kutelle kolome liri.
Alikuwa mtu mwema; naye pamoja na jamaa yake yote walimcha Mungu; alikuwa anafanya mengi kusaidia maskini wa Kiyahudi na alikuwa anasali daima.
3 Kubi nikoro kutir nin wui, ayene kanang nanya namoro alau gono kadura Kutelle din cinu udak kitime. Gono kadure woroghe, “Konoloyus!”
Yapata saa tisa mchana, aliona dhahiri katika maono malaika wa Mungu akiingia ndani na kumwambia, “Kornelio!”
4 Konoliyus yenje gono kadure fiu daghe aworo, “Inyaghari unit udya?” Gono kadure woroghe, “Nlirafe nin nimon ile na udin filluzunu akimon mun nghana kite nafo unizun lizzinu inbun Kutelle.
Kornelio alimkodolea macho huyo malaika kwa hofu, akamwambia, “Kuna nini Mheshimiwa?” Huyo malaika akamwambia, “Mungu amezipokea sala na sadaka zako kwa maskini.
5 Nene to anit udu kagbirin Joppa idak nin nit lissame Simon, urika na idin kitin yiccughe tutung Bitrus.
Sasa, watume watu Yopa wakamwite mtu mmoja aitwaye Simoni, kwa jina lingine Petro.
6 Nin Kutana lissame Simon, urika na kilari me din biu kurawa.”
Yeye yumo nyumbani kwa Simoni mtengenezaji wa ngozi ambaye nyumba yake iko karibu na bahari.”
7 Na gono kadura Kutellen mala uliru ninghe, Koloniyus yiccila acin awaba kilarime, nin kusojako na kuwadi su Kutelle usujada nanya nasoja na iwa dighe katwa.
Huyo malaika aliyesema hayo alipokwisha kwenda zake, Kornelio aliwaita watumishi wawili wa nyumbani na mmoja wa askari zake ambaye alikuwa mcha Mungu,
8 Konoliyus belle nani vat nimon ilen na isu anin tonani udu u Joppa.
akawaeleza yote yaliyotukia, akawatuma Yopa.
9 Nin liri liba nin kubi nikoro kutocin, na iwadi nanya ncin mine inin da kupo kippin, Bitrus ghana kulari kitene ati nlira.
Kesho yake, hao watu watatu wakiwa bado safarini, lakini karibu kufika Yopa, Petro alipanda juu ya paa la nyumba yapata saa sita mchana ili kusali.
10 Kupkon da anin yita ninsu li nimonmon, na anite wadi likanju nimoli, ayene amoro alau,
Aliona njaa, akatamani kupata chakula. Chakula kilipokuwa kinatayarishwa, alipatwa na usingizi mzito akaona maono.
11 anin yene kitenen puno kidowo nin nimonmon nafo kukuzunntolsu, imone gbardang nafo kukuzu ucin tolu kutiin, iwa tolti kunin nin nasari anasme.
Aliona mbingu zimefunguliwa na kitu kama shuka kubwa inateremshwa chini ikiwa imeshikwa pembe zake nne.
12 Nanya kunin vat ninawan tene nabunu anas nin nimon ile na idin kurtu kutiin, a ayiin kitene kani.
Ndani ya shuka hiyo kulikuwa na kila aina ya wanyama: wanyama wenye miguu minne, wanyama watambaao na ndege wa angani.
13 Liwui tunna li lirina ninghe: “Fita Bitrus, ubo uli.”
Akasikia sauti ikimwambia: “Petro, amka uchinje, ule!”
14 Bitrus woro, “Na nanera ba, Cikilari; nan sa leu imon na idi nanzang sa dinon ba.”
Petro akajibu, “La, Bwana; mimi sijaonja kamwe chochote ambacho ni najisi au kichafu.”
15 Ama liwuiye daa kitime umba: “Ile imon na Kutelle nwesse yenju uwa woro idinin dinong.”
Ile sauti ikasikika tena ikimwambia: “Usiviite najisi vitu ambavyo Mungu amevitakasa!”
16 Na ayine ile imone so titat kiteene itunna ighantina kugbetue udu kitene kani.
Jambo hili lilifanyika mara tatu, kisha ile shuka ikarudishwa juu mbinguni.
17 Nene na Bitrus nyene amoron nwui anin din kpilizu nyanghar adi, awa ba na Kaniliyos ntoo nani ida yisina kibulung ghe, na itirino kilari kaa na aduku.
Petro alipokuwa bado anashangaa juu ya maana ya hilo maono alilokuwa ameliona, wale watu waliotumwa na Kornelio, baada ya kuigundua nyumba ya Simoni, walifika mlangoni,
18 Inin yicila itirino sa Siman, ulenge na idin yicu ghe Bitrus, sosin kikane.
Wakaita kwa sauti: “Je, kuna mgeni humu aitwaye Simoni Petro?”
19 Na Bitrus se wa din kpilzu kitene na moron wui ye, Uruhu belin ghe, “Yene, anit atat nalime din piziru fi.
Petro alikuwa bado anajaribu kuelewa lile maono, na hapo Roho akamwambia, “Sikiliza! kuna watu watatu hapa, wanakutafuta.
20 Fitaa utolu unin nyaa ligowe nan ghinu, na uwann nari unyiu ligowe nan ghinu, na uwan nari unyiu ligowe nan ghinu ba, bara nan too nani.”
Shuka upesi na wala usisite kwenda pamoja nao kwa maana ni mimi niliyewatuma.”
21 Nani Bitrus se tolo kadase ade see anit aworo ani, “Mere ule na idin pizirughe. Inyangharin ndaa ninghinu?”
Basi, Petro akateremka chini, akawaambia hao watu, “Mimi ndiye mnayemtafuta. Kwa nini mmekuja?”
22 I woro, “Unan buun ligozin nasoja likoolt nin lisa Kaniliyos, unit ulau nin lee na adin su Kutelle usujada, unitari ule na vat nmin na Yahudawa din liru litime, Kutelle wa tuu gono kadura me kilau ucindu kilari me, adan lanza kadura nnuzu kitife.”
Wao wakamjibu, “Jemadari Kornelio ambaye ni mtu mwema, mcha Mungu na mwenye kuheshimika mbele ya Wayahudi wote ametutuma. Aliambiwa na malaika mtakatifu akualike nyumbani kwake ili asikilize chochote ulicho nacho cha kusema.”
23 Bitrus se yicala ani ipiru nin nati isoo ligowe nan ghe. Ukurtunun kui ye afita anyaa ligowe nin ghe, nin nan nuwuna nnuzun Jopa na iwufu ghe.
Petro akawaalika ndani, akawapa mahali pa kulala usiku ule. Kesho yake, Petro alianza safari pamoja nao, na baadhi ya ndugu wa huko Yopa walifuatana naye.
24 Nin Shantung kui me idaa Usizeriya. Kaniliyos wa din ncaa mine, awa dak ligowe nin likura a adindong asusut me.
Siku ya pili yake, walifika Kaisarea na huko Kornelio alikuwa anawangojea pamoja na jamaa na marafiki aliokuwa amewaalika.
25 Kubi koo na Bitrus se npira, Kaniliyos tumuno na bunu fe atighe gongong.
Petro alipokuwa anaingia, Kornelio alitoka nje kumlaki, akapiga magoti mbele yake na kuinama chini kabisa.
26 Ama Bitrus se fya ghe aworo, “Yisina; Meng wang litine unitari.”
Lakini Petro alimwinua, akamwambia, “Simama, kwa maana mimi ni binadamu tu.”
27 Kubi koo na Bitrus wa din liru ninghe, a pira nanya a ssee anit gbardang sosin ligowe.
Petro aliendelea kuongea na Kornelio wakiwa wanaingia nyumbani ambamo aliwakuta watu wengi wamekusanyika.
28 Aworo ani, “Anun atimine yiru na ucaun Kuyahudawa munu liti nin, sa a doo kitin mong nnuzu mmong mmin. Ama Kutelle na dursoi na nwa yicila umong unit ananni sa unan dinong.
Petro akawaambia, “Ninyi wenyewe mnajua kwamba Myahudi yeyote amekatazwa na Sheria yake ya dini kushirikiana na watu wa mataifa mengine. Lakini Mungu amenijulisha nisimfikirie mtu yeyote kuwa najisi au mchafu.
29 Un naren taa ndaa ba manyardang, na uwa tuu ndak. Bara nani ntirin fi uminin too ndak.”
Kwa sababu hiyo, mliponiita nimekuja bila kusita. Basi, nawaulizeni: kwa nini mmeniita?”
30 Kaniliyos woro, “Ayiri anas na ana kata kubi fo kone, Nwa din nlira kubi likure sa irum nya kilari ning; nnin yene, unit yisin nbun ning nin nimon iboo pas.
Kornelio akasema, “Siku tatu zilizopita saa kama hii, saa tisa alasiri, nilikuwa nikisali chumbani mwangu. Ghafla, mtu aliyekuwa amevaa mavazi yenye kun'gaa alisimama mbele yangu,
31 Aworo, 'Kaniliyos, Kutelle nlanza nlira fe, ile imon na udin filzinu ni kimon ntaa Kutelle koni nlizino ning fi.
akasema: Kornelio! Sala yako na sadaka zako kwa maskini vimekubaliwa na Mungu.
32 Too umong udu Ujopa, iyicila fi umong unit unan lisa Simon, ule wang na idin yicighe Bitrus, kupopo ngau kuli.'
Mtume mtu Yopa akamwite mtu mmoja aitwaye Simoni, kwa jina lingine Petroi; yuko nyumbani kwa Simoni mtengenezaji wa ngozi karibu na bahari.
33 Kube ntunna ntoo iyicila fi. Ucaun na udaa. Nene na vat bite di kikane nbun Kutelle, ti lanza vat nile imon na Cikilari na dursufi ubelin.”
Kwa hiyo nilikutumia ujumbe bila kuchelewa, nawe umefanya vyema kuja. Sasa, sisi tuko mbele ya Mungu, kusikiliza chochote ambacho bwana amekuamuru kusema.”
34 Bitrus puu no unuu me aworo, “Kidegene, Nyinno na Kutelle din feru ba.
Hapo Petro akaanza kusema: “Sasa nimetambua kwamba hakika Mungu hana ubaguzi.
35 Nnani, nyan vat nmin Kutelle din sesu vat na nit ale na idin suu ghe usujada nin adadu alau.
Mtu wa taifa lolote anayemcha Mungu na kutenda haki anapokelewa naye.
36 Iyiru kadura kaa na ana tuu udu kiti nat Nisraila, kubi koo na awa belin uliru umang nyan Yesu Kristi, ulenge amere Cikilarin vat-
Huu ndio ule ujumbe Mungu alioupeleka kwa watu wa Israeli, akitangaza Habari Njema iletayo amani kwa njia ya Yesu Kristo ambaye ni Bwana wa wote.
37 anun atimine yiru ile imon na ina su, ile na iwa se vat nyan Judiya, ucizinue Ngaliliya, nkatun Baptisma Nyuhana na awa belin;
Ninyi mnajua jambo lililotukia katika nchi yote ya Wayahudi kuanzia Galilaya baada ya ule ubatizo aliohubiri Yohane.
38 Imone kitenen Yesu Nnazaret, na Kutelle wa kusu ghe nin Ruhu Ulau nin na gang. Anyaa atinnang su kataa kacine nin shizinu na le na ibilis wa nodin nani, Kutelle wa di ligowe nin ghe.
Mnajua Yesu wa Nazareti na jinsi Mungu alivyomteua kwa kummiminia Roho Mtakatifu na nguvu. Mungu alikuwa pamoja naye; yeye alikwenda huko na huko akitenda mema na kuwaponya wote waliokuwa wamevamiwa na Ibilisi.
39 Arik anan niyizi ibaari nvat nimon ile na anan nmin na Yahudawa nin Urushalima-Yesu ulele na iwa molu ghe, ibana ghe kitene ku ca.
Sisi ni mashahidi wa mambo yote aliyotenda katika nchi ya Wayahudi na katika Yerusalemu. Walimuua kwa kumtundika msalabani;
40 Unit ulele Kutelle fya ghe nya liri lin tat anakpa ghe anun nan yinin ghe,
lakini Mungu alimfufua siku ya tatu, akamfanya aonekane
41 na nvat nanitere ba, ama udu nanit ashaida alenge na Kutelle wa fere nani nworsu-arik atibite, ale natiwa li tisono nan ghe kimal nfitu me nkul.
si kwa watu wote ila kwa wale Mungu aliokwisha wachagua wawe mashahidi wake, yaani sisi tuliokula na kunywa pamoja naye baada ya kufufuka kwake kutoka wafu.
42 Awa ti nari, tisu uwaazi kiti nanit, ti kunu ti bellin nani ulelere, Kutelle na fere, usughe ushara kiti na nan lai, nin na nan nkul.
Alituamuru kuihubiri Habari Njema kwa watu wote na kushuhudia kwamba yeye ndiye aliyeteuliwa na Mungu awe Mwamuzi wa wazima na wafu.
43 Viti mere vat, na anabawa wani ushaida, bara kogha na ayinna ninghe anan sere usurtu nanya kulapi unuzu lissa me.”
Manabii wote waliongea juu yake kwamba kila mtu atakayemwamini atasamehewa dhambi zake zote kwa jina lake.”
44 A bitrus dutu nbellu nile imone Uruhu Ulau tolo kitene nati nalenge vat na iwa di nlanzu, uliru me.
Wakati Petro alipokuwa bado anasema maneno hayo, Roho Mtakatifu aliwashukia wote waliokuwa wanasikiliza ujumbe huo.
45 Anit alenge na inung wandi nanya na nan kalizu nacunu-vat nalenge na iwa dak ligowe nan Bitrus fiu kiffo nani bara ufillu Nruhu Ulau we wa tolu wang kitene na wurumi.
Wale Wayahudi waumini waliokuja pamoja na Petro kutoka Yopa walishangaa kuona kuwa Mungu aliwamiminia zawadi ya Roho Mtakatifu watu wa mataifa mengine pia;
46 Bara iwa lanza Awurumi ane dinsu uliru nin ton tilem ugang izazina Kutelle. Bitrus kauwa a woro,
maana waliwasikia wakiongea kwa lugha mbalimbali wakimtukuza Mungu. Hapo Petro akasema,
47 “Umong wasa anaza nin mmyen nworu na iwa shintin anit alelena isere Uruhu Ulau we umunu arike ku wangha?”
“Watu hawa wamempokea Roho Mtakatifu kama sisi wenyewe tulivyompokea. Je, kuna yeyote atakayeweza kuwazuia wasibatizwe kwa maji?”
48 Atunna ataa ishinto nani mmyen nanya lissan Yesu Kristi. Ifoghe acara aso ligowe nanghinu uduru among ayiri gbardang.
Basi, akaamuru wabatizwe kwa jina la Yesu Kristo. Kisha wakamwomba akae nao kwa siku chache.

< Katwa Nono Katwa 10 >