< 2 Timotawus 4 >

1 Ndin ni nliru ulele nin likara nbun Kutelle nin Kristi Yesu, ule na aba gucu anan lai nin nanan kul, bara udak me nin kipin tigome:
Ninakupa agizo hili lenye uzito mbele za Mungu na Kristo Yesu, atakaye wahukumu walio hai na wafu, na kwa sababu ya kufunuliwa kwake na Ufalme wake:
2 Su uwazi nliru, so nin shiri, sa kubi di sa na kubi duku ba kpada, gbara, taa kubun, vat nin kanyiri nsuwe nin teru kibinai nanya ndursuzu.
Hubiri Neno. Uwe tayari kwa wakati ufaao na usiofaa. Waambie watu dhambi zao, kemea, himiza, kwa uvumilivu wote na mafundisho.
3 Bara kubi din cinu, na anit ma teru nibinai nin ndursuzu ucine ba nani iba na pitiru atimine anan dursuzu kiti alenge na iba shogulu nu nanya nlanzu mine.
Kwa maana wakati utakuja ambao watu hawatachukuliana na mafundisho ya kweli. Badala yake, watajitafutia walimu wa kufundisha kulingana na tamaa zao. kwa njia hii masikio yao yatakuwa yametekenywa.
4 Iba kpiliu ulanzu mine kiti nlanzu kidegen, iba na kpillu kusari nlanzu nabin ghari.
Wataacha kusikiliza mafundisho ya kweli, na kugeukia hadithi.
5 Amma fe nonko kibinai nanya nimon vat. Tere kibinai nanya nniu; su katwa nnan bellun nliru Kutelle; kullo katwa fe.
Lakini wewe uwe mwaminifu katika mambo yote, vumilia magumu, fanya kazi ya mwinjilisti; timiza huduma yako.
6 Bara meng ina mallu ugutu niyi. Kubi in nyiu nighe nmal dak.
Kwa maana mimi tayari nimekwisha kumiminwa. Muda wa kuondoka kwangu umewadia.
7 Nnasu likum licine. Nna min uyinnu sa uyenu nighe.
Nimeshindana katika haki, Mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda.
8 Ina malu uciuyi litapa katwa kacine, longo na Cikilari, unan wucu ucine, ama niyi liyiri lole. Ana meng usanin ba, umunu alenge na ima yitu nin su in saku ndak me.
Taji ya haki imewekwa kwa ajili yangu, ambayo Bwana, anayehukumu kwa haki, atanipa siku ile. Na siyo kwangu tu bali pia kwa wote wanaongojea kwa shauku kuonekana kwake.
9 Yita nin kanyeri udak kiti nighe mas.
Jitahidi kuja kwagu haraka.
10 Bara Dimas na sunni, dinin su nlenge uyie amini na nya udu utasalanika. Kariskis na do ugalatiya, Titus uni nado udalmatiya. (aiōn g165)
Kwa kuwa Dema ameniacha. Anaupenda ulimwengu wa sasa na amekwenda Thesalonike, Kreseni alikwenda Galatia, na Tito alikwenda Dalmatia. (aiōn g165)
11 Luka ri cas di nimi. Yira Markus ku udak ligowe ninghe, bara adinin ampani kiti nighe nanya katwa we.
Luka tu ndiye yuko pamoja nami. Umchukue Marko uje naye kwani yeye ni muhimu kwangu katika huduma.
12 Nna tuu Tikikus ku in Afisas.
Nimemtuma Tikiko Efeso.
13 Ugudum nighe nann nna sun Ntaruwas nacara karbus, mino unin asa uba dak, umunu affa ninyerte, Massaman affe vat.
Lile joho ambalo nililiacha Troa kwa Karpo, utakapokuja lilete, pamoja na vile vitabu hasa vile vya ngozi.
14 Iskandari unan kitel nikoro iboo nasu likara linanzang gbardang liti nighe Cikilari ba kurtun ghe nafo na ame nasuzu.
Alekizanda mfua chuma alinitendea maovu mengi. Bwana atamlipa kulingana na matendo yake.
15 Fe wang yenje Ucinfe ninghe, bara adi nivira nin liru bite.
Nawe pia jihadhari naye, kwani aliyapinga sana maneno yetu.
16 Nin kusu liti nighe un cizinue, na umong wa yisin nin mie ba. Nani, vat nanite wa su ni. Na Kutelle nwa batiza ileli imone nati mine ba.
Katika utetezi wangu wa kwanza, hakuna mtu yeyote aliyesimama pamoja nami, badala yake, kila mmoja aliniacha. Mungu asiwahesabie hatia.
17 Amma Cikilare wa yisin likot nighe atayi likara, bara, nnuzu kiti nighe, bara ubellu nlirue nan se ukullu vat, nwurumi nan se ulanzu. Nwase utucu nnuu nzakki.
Lakini Bwana alisimama pamoja nami, akanitia nguvu ili kwamba kupitia kwangu, neno linenwe kwa ukamilifu na mataifa wapate kusikia. Niliokolewa katika kinywa cha Simba.
18 Cikilari ma tucui nanyan ko lome likara linanzang, ama nin ciu yi bara kipin tigo me kitene kani. Kiti mere ngongong so ku udu sa ligang. Uso nani. (aiōn g165)
Bwana ataniepusha na matendo yote maovu na kuniokoa kwa ajili ya ufalme wake wa mbinguni. Utukufu uwe kwake milele na milele. Amen (aiōn g165)
19 Lissoi Briskila ku nin Akila, nin na nan kilarin anisifirus.
Msalimie Priska, Akila na nyumba ya Onesiforo.
20 Erasitus wa lawa Nkorontus, Amma nwasun Tirifehimus ku Nmilatuss nin nkonu.
Erasto alibaki huko Korintho, lakini Trifimo nilimuacha Mileto akiwa mgonjwa.
21 Yita nin lissufi, pudens wang nin linus, claudia nin linuana vat din lissufi.
Fanya hima uje kabla ya kipindi cha baridi. Eubulo anakusalimu, pia Pude, Lino, Claudia na ndugu wote.
22 Na cikilari so nin Nruhu fe. Na ubolu Kutelle so nin fi.
Mungu awe pamoja na roho yako, Neema iwe nawe.

< 2 Timotawus 4 >